Thursday, May 14, 2015

MSAADA KWA JAMII NI MOJA YA HUDUMA KUTOKA NIC

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe Gulam Hafeez akikagua vifaa vya watoto wenye ulemavu wa Ngozi, Wasioona na kusikia baada ya kukabidhiwa na Meneja wa NIC tawi la Shinyanga Bi Halima Makange.

Meneja wa NIC Tawi la Shinyanga Bi Halima Makange akitoa vifaa vya huoni hafifu katika kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu wa ngozi, wasioona na kusikia cha Buhangija Shinyanga, anayepokea msaada huo ni Msimamizi wa kituo hicho Mwl Peter Ajali.

Meneja Wa NIC Tawi la Shinyanga Bi Halima Makange akimuonesha Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe Gulam Hafeez vifaa vya watoto wenye ulemavu wa Ngozi, wasioona na kusikia katikati ni Mlezi wa Kituo hicho Mwl Peter Ajali Akishuhudia .

Mtaalamu wa Macho Fani ya Uoni hafifu kutoka Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga, Dr. Ntoke Sospeter Wilson akiwaelezea watoto hao namna ya kutumia darubini Kiona Mbali.

Meneja wa NIC Tawi la Shinyanga akiwa katikati ya watoto wenye ulemavu wa Ngozi wa ngozi, wasioona na kusikia wakiwa wakijaribu kutumia kifaa cha Darubini Kiona Mbali katika kituo hicho Mjini Shinyanga.

No comments: