Monday, March 23, 2015

MAFUNZO YA BIMA KWA CHAMA CHA WAFANYAKAZI WA USAFIRISHAJI KWA NJIA YA BARABARA TANZANIA (TAROTWU).


Chama cha wafanyakazi wa usafirishaji kwa njia ya barabara Tanzania (TAROTWU) kimeweka mkakati wa kuhakikisha kwamba wafanyakazi wa sekta ya usafirishaji wanapewa elimu juu ya Bima na kuhamasishwa kukata Bima ya ajali ili kujiwekea kinga. 

TAROTWU ikiwasilisha risala yao kwa mgeni rasmi Rose Lutu Lawa,  ambaye alimuwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) chama hicho kilisema mkakati wao ni kuhakikisha wafanyakazi wa sekta ya usafirishaji wananufaika na kupata maslahi bora ili kuondokana na matatizo yanayotokana na changamoto zilizopo katika soko la utandawazi na kuimarisha uchumi wa Taifa.

Waliongeza kuwa mkakati wao pia ni kuunda kamati za Elimu kila mkoa ili zishirikiane na idara ya kazi, CMA, SUMATRA, BIMA NIC na vyuop vya VETA nchini na wadau wengine katika kuelimisha wafanyakazi wakiwemo madereva malori, mabasi ya abiria, bodaboda, bajaji, mafundi wa magari na makondakta, mawakala wa mabasi na malori ya mizigo na mautingo 

Mgeni rasmi katika mafunzo hayo alikuwa mwakilishi wa mkurugenzi mtendaji  wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Bi. Rose Lutu Lawa (watatu kushoto). 

Mr. Mabula akifungua mkutano maalum wa wafanyakazi katika ukumbi wa chuo cha VETA Dodoma tarehe 19/03/2015.


Wanachama wa TAROTWU wakifuatilia mafunzo.






No comments: