Friday, November 28, 2014
MKUTANO WA MENEJIMENTI YA SHIRIKA LA BIMA ULIOFANYIKA KATIKA HOTELI YA GIRAFFE ILIYOPO DAR ES SALAAM
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika akifungua Mkutano wa Menejimenti
Mkurugenzi wa Bima za Maisha akifungua kikao kwa "SALA" maalum.
Wajumbe wakipitia taarifa kabla hazijawasilishwa kwenye kikao.
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala akitoa mchango wake.
Chief Meneja wa ICT akiwasilisha hoja Mkutanoni
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala Bi. Anne Mbughuni akiwasilisha hoja Mkutanoni
Mkurugenzi wa Bima zisizo za Misha Bw. Kura Boniface akisisitiza jambo.
Meneja wa Mkoa wa Dodoma Bw. Lugano Stanton
akichangia katika moja ya hoja zilizo wasilishwa kwenye mkutano.
Kaimu Meneja wa Uwekezaji na Mipango Bi. Sabra Abdul-Rahman
akiwasilisha bajeti ya shirika ya 2015-16
Kaimu Meneja wa Uwekezaji na Mipango Bi. Sabra Abdul-Rahman
akiwasilisha jambo.
Meneja wa Bima za Maisha Bw. Henry Mwalwisi akitoa Mchango wake
Meneja wa Mkoa wa Bukoba Bw. Mazagwa naye
akichangia jambo kwenye hoja iliyowasilishwa mkutanoni.
Meneja wa Bima za Maisha Bw. Isihaka Kibamba akitoa Mchango wake
Mkurugenzi wa Masoko Bw. Henry Machoke akichangia katika
moja ya hoja zilizo wasilishwa Mkutanoni
Mkurugenzi wa Audit Bw. Gosbert Kafanabo akiwasilisha hoja Mkutanoni
Meneja wa Mkoa wa Tawi la Ubungo Bw. Segeja Mabula naye
akitoa mchango wake kwenye hoja iliyowasilishwa mkutanoni.
Wakurugenzi wa Masoko na Audit kwa pamoja
wakichangia jambo kwenye hoja iliyowasilishwa mkutanoni.
Mkurugenzi Mtendaji Bw. Justine Mwandu akifafanua jambo Mkutanoni
Friday, June 27, 2014
MKURUGENZI MTENDAJI NA MAOFISA WA JUU WAPEWA MAFUNZO YA MFUMO MPYA WA TEHAMA GENISYS CONFIGURATOR
Mkurugenzi Mtendaji na timu yake amaliza kupata maelekezo ya mwisho juu ya mfumo mpya TEHAMA unavyofanya kazi.
(Kutoka kushoto kwenda kulia)
Mkurugenzi Mtendaji Bw. Justine Mwandu, Bw. Gosbert Kafanabo Mkuu wa Idara ya Ukaguzi wa mahesabu ya ndani , Bw. Deepak Mtaalam wa Mtambo mpya wa TEHAMA kutoka India ,
Bi. Anne Mbughuni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Hamza Ngereza (Mwanafunzi katika majaribio) Msaidizi idara ya TEHAMA na Bw. Mohamed Rashid Mtaalamu wa ndani wa mfumo mpya wa
TEHAMA GENISYS CONFIGURATOR
Saturday, June 21, 2014
Friday, June 6, 2014
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MH. SAADA MKUYA SALUM (MBUNGE) ALIYOIWASILISHA BUNGENI AKIWASILISHA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA KWA MWAKA 2014/15
WAZIRI WA FEDHA MH. SAADA MKUYA SALUM (MBUNGE)
HAPA TUNAKULETEA SEHEMU YA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA ALIPOGUSIA MASUALA YA BIMA NA MUSTAKABALI WA SHIRIKA LA BIMA LA TAIFA (NIC)
Huduma za Bima
Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za
Bima – TIRA
99. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/14, Wizara kupitia
Mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima imekamilisha na kutoa Mkakati wa
Kuendeleza Bima ya Watu wa Kipato cha Chini - National Micro Insurance Strategy
2014-2017. Aidha, hadi kufikia Aprili 2014, kampuni 30, madalali 100 na
mawakala 500 wa bima alisajiliwa. Vile vile, mauzo ya bima yaliongezeka kutoka
shilingi bilioni 406.7 mwaka 2012/13 hadi kufikia shilingi bilioni 481.7 sawa
na ongezeko la asilimia 18.5.
100. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2014/15,
TIRA
inatarajia kutekeleza yafuatayo: kuendelea na maandalizi ya kufungua ofisi
nyingine za kanda;kuendelea na utaratibu wa uoanishaji sheria na kanuni za soko
la bima katika eneo la Afrika Mashariki na lile la nchi za SADC; kuendelea na
tafiti za bima ya kilimo, mifugo, pamoja na bima za watu wa kipato cha chini; na
kukamilisha taratibu za kuanzisha bima ya Takaful.
Shirika la Bima la Taifa – NIC
101.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/14, Wizara ilikamilisha urekebishaji wa
Shirika la Bima la Taifa na usimikaji wa mfumo wa TEHAMA kwa lengo la kuongeza
ufanisi. Utendaji wa Shirika kibiashara uliendelea kuimarika ambapo mapato ya
bima yaliongezeka kutoka shilingi bilioni 27.38 mwaka 2012, hadi kufikia
shilingi bilioni 31.53 mwaka 2013, ongezeko hilo ni sawa na asilimia 15. Mapato
haya yalitokana na makusanyo ya bima za mtawanyo, vitega uchumi na mapato
mengine.
102. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia
Desemba 2013, NIC ililipa madai ya wateja ya shilingi bilioni 8.31. Malipo hayo
yalilipwa kwa wateja wa bima za maisha kiasi cha shilingi bilioni 5.71 na
wateja wa bima za kawaida kiasi cha shilingi bilioni 2.60.
103. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2014/15,
Wizara itaendelea na mkakati wa kuligawa Shirika katika kampuni mbili, ambayo
ni Kampuni ya Bima za Maisha na Kampuni ya Bima za Kawaida. Aidha, Shirika
litaendelea na mkakati wa kujitangaza zaidi na kuongeza biashara kwa kubuni
bima mpya zinazokidhi mahitaji ya wananchi.
Kwa kusoma hotuba yote nenda kwenye muelekeo huu;
source: Ministry of Finance
Subscribe to:
Posts (Atom)




