Wednesday, June 24, 2015

MBUNGE WA GEITA AFARIKI DUNIA.





Kikao cha bunge kimeahirishwa hadi kesho saa 3 Asubuhi kutokana na msiba wa  Mbunge wa Geita (CCM), Donald Max (58) amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.
Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema kuwa mbunge huyo (pichani) alifariki jana saa 12.00 jioni katika hospitali hiyo.Ndugai alisema Max alikuwa mahututi kwa kipindi cha takribani miaka miwili iliyopita na mwili wa marehemu unatarajiwa kuzikwa Jumamosi Juni 27 jijini Dar es salaam. 
Max alizaliwa Mei 22 mwaka 1957 na kusoma katika Shule ya Msingi ya Salvatorian Convent na baadaye kujiunga na Shule ya Sekondari ya Azania mwaka 1971 hadi mwaka 1974.
Mwaka 1980 alikwenda nchini Urusi na kusoma kozi ya ufundi katika Chuo cha Ufundi cha Roston on Don kabla ya kujiunga na Taasisi ya Volgograd Polytechnical nchini humo na kutunukiwa Shahada ya Uzamili katika Uhandisi.
Mungu ampumzishe mahali pema peponi.

No comments: